Wafanyabiashara wagawanyika

Mkazi wa mjini Moshi akipita katikati eneo la Kariakoo mji humo huku maduka yaki yamefungwa baada ya jumuiya ya wafanya biashara Mkoa wa Kilimanjaro kuwamasishana kuyafunga wakipinga kutumia mashine za EFD na kupandishwa kwa kodi ya mapato, mkoani humo jana. Picha na Dionis Nyato

Wauzaji na wamiliki wa maduka maeneo ya Mwanjelwa, Uhindini na Sido mkoani Mbeya jana waliwalaumu viongozi wao kwa kuwashinikiza kuyafunga maduka bila kutoa sababu za msingi na kuwasababishia hasara.
Wamesema tabia ya kufunga maduka inawaathiri wao na wateja badala ya Serikali inayolaumiwa.
Wakizungumza kwa sharti la kutotajwa majina yao, wafanyabiashara hao walisema, viongozi wao wanawalazimisha kuyafunga maduka na kwamba atakayefungua atalipishwa Sh50,000.

No comments:

Post a Comment