Magufuli afyeka mishahara ya vigogo



Rais John Magufuli 
By Rehema Matowo, Mwananchi rmatowo@mwananchi.co.tz

Chato. Rais John Magufuli ametangaza kiama cha watendaji wakuu wa mashirika na taasisi za umma waliojipangia mishahara minono kufikia Sh40 milioni akiahidi kuifyeka hadi kiwango kisichozidi Sh15 milioni kuanzia bajeti ijayo ya fedha ikiwa ni punguzo la asilimia 63.

“Atakayeona kiwango hicho ni kidogo namshauri aanze kutafuta kazi sehemu nyingine kwa sababu hatuwezi kuendelea kulipana mishahara minono kiasi hicho katikati ya wananchi wanaoishi katika lindi la umaskini,” alisema Rais Magufuli na kushangiliwa kwa nguvu na wananchi.

Akihutubia mkutano wa hadhara katika Uwanja wa Mazaina mjini Chato jana katika siku yake ya kwanza nyumbani kwake tangu achaguliwe kushika wadhifa huo, Rais Magufuli aliahidi kupandisha mishahara ya watumishi wa chini ili kupunguza tofauti ya kipato kati yao na wale wa juu. “Katika Serikali ninayoongoza, sitegemei kumlipa mtumishi zaidi ya Sh15 milioni; tayari nimeunda tume kushughulikia suala hilo,” alisema na kuongeza: “Kiwango tunachopunguza kutoka kwenye mishahara minono ya wakubwa tutawaongezea watumishi wa chini ambao baadhi wanalipwa mishahara midogo inayoanzia Sh300, 000.

Kichupa cha leo.Amini - Hawajui Official Video

US Agency Stops Aid to Tanzania

By Mwakilishi | Tue, 03/29/2016 12:10PM -0400

Tanzanian President John Magufuli (second left) and Zanzibar's newly elected President Ali Mohamed Shein (second right)...
A US international development agency has suspended its partnership with Tanzania, citing flawed Zanzibar elections and the draconian Cybercrime Act.
The move by the board of directors of Millennium Challenge Corporation (MCC) means that Tanzania will not be receiving an envisioned $472 million in funding for electricity projects.
In addition to complaining that Tanzania had gone forward with a flawed Zanzibar electoral process “despite the repeated concerns of the US government,” the MCC board said Tanzanian authorities had failed to ensure that the country's Cybercrimes Act “would not be used to limit freedom of expression and association.”
The US suspension-of-aid notification cites “arrests made during the elections” in Zanzibar as an indication of the Tanzania government having “engaged in apattern of actions inconsistent with MCC'seligibility criteria.”
“MCC’s model has a partner country’s commitment to democracy and free and fair elections at its core,” the directors' statement said.
Tanzania had previously been a favoured recipient of US development aid.
The country qualified in 2008 for nearly $700 million in US assistance for road, water and energy projects.
That ranked at the time as the largest single funding stream approved by MCC, an agency that makes development aid contingent on countries' compliance with a set of conditions involving human rights, governance and free-market economic policies.
- Nation.co.ke

Native Kenyan strives for success in Kansas, Missouri

Posted by  

Eileen
Print Friendly
At 17, Eileen Lusamukha stepped onto American soil for the first time.
Now, 16 years later, she has overcome obstacles to earn a bachelor’s degree while holding down a full-time job at Belton’s IHOP.
“I would never want to take advantage of my opportunity,” Lusamukha said. “Being a foreigner and immigrant, a lot of people in undeveloped countries would want to be in my position, and that’s why I work so hard.”
Lusamukha often waits on the members of the Ray-Pec Optimist Club, which meets weekly at IHOP. President Ed Russell said Lusamukha’s work ethic shines through in her attentiveness to details like the members’ drink preferences.
So, at a recent meeting, the members of the club asked Lusamukha to share her story with them.
“We thought it’d be good for all of our members to hear straight from her what she’s done and what she’s gone through,” Russell said.
For the members, it was the first time they learned their waitress was originally from Kenya.
In her country, English is one of the official languages, so Lusamukha had a good grasp of it when her family arrived on the East Coast in 2000.
Still, a new culture and different dialect of English was challenging to adjust to.
“Everything was difficult,” she said. “School was difficult, and people pronounce things different than the British.”
Three years after she arrived with her family, her parents moved back to Kenya. But Lusamukha stayed, choosing to remain in a foreign country, far from her immediate family.
She wanted to stay to achieve her goal of graduating from college and pursuing a master’s degree, so she moved to Kansas City, where extended family lived.
“Initially I went to college and flunked out. (My) English papers had a lot of grammatical mistakes, and it just got very frustrating for me because I’m very driven. I strive to do my best in everything,” Lusamukha said.
But she kept at it. Eventually she enrolled at UMKC to pursue an international studies degree. She held down her job at Belton’s IHOP despite a hectic schedule, and she successfully applied for dual citizenship in Kenya and the United States.
“I like learning about other cultures … and I’ve been that way ever since I was little,” she said.
While taking classes at UMKC, a typical day for Lusamukha began at 5:30 a.m. at IHOP for a full shift. After getting off in the early afternoon, she completed homework before her first class at 3 or 4 p.m. and then attended classes until as late as 10 p.m.
“It was hectic, but like I said I’m here alone,” she said. “I have bills to pay so that’s what I have to do.”
Her perseverance and ambitious attitude eventually paid off. Last month she graduated with her bachelor’s degree, and soon she’ll begin pursuing a master’s degree in business.
A few days after she spoke to the Optimist Club, Lusamukha spoke about her country. She said Kenya was once one of the more peaceful in eastern Africa but now must confront radical extremism following recent attacks. A September 2013 attack on a mall in her home city of Nairobi left 69 dead and injured 175.
And the Kenyan economy, she said, has faltered recently due to ongoing political corruption.
“We do have a Constitution but it’s not followed,” Lusamukha said, adding presidential tenures are supposed to be limited to two five-year terms. But former president Daniel Moi took office in 1979 and retained the position until 2002.
“The middle class should not be struggling, but in my country they’re struggling. They have to pick and choose what they’re going to pay for bills, and the cost of living there is so high,” she said.
Though she visits Kenya often, she doesn’t plan to move back.
“This is where I became an adult, so I feel like it would be so hard to go back to that,” Lusamukha said, adding that she is often surprised by the ignorance that some Americans have about Kenya.
“The biggest problem I have about America is the fact that everybody, (asks) me silly questions,” Lusamukha said. “They ask, ‘Did you live in a jungle?’ I did not grow up with lions in my backyard, but that’s the misconception they have.”
She continued by saying poverty is not universal in her country, but it can be more damaging than in the U.S. because her home country lacks the strong federal assistance programs found here.
“People there, when they tell you they’re starving, they’re actually starving. But it’s not all of Africa.”
She added that without money, continuing education is impossible in Kenya. “There’s nothing like financial aid.”
One of her goals is to use her international studies degree to travel the world and serve as a translator, to bring awareness to a country many Westerners know little about.
Lusamukha’s journey has shown her the importance of education, and now she says she tries to inspire younger people to continue on in school.
“I was luckier than some of my friends. I still have that in the back of my mind,” she said. “I never want to sit here and waste time and waste opportunities given to me.”
-The Democrat Missourian

Uchambuzi wa Humphrey Polepole Kuhusu Marekani Kusitisha Msaada wa Mabilioni ya Pesa na Shughuli zake Tanzania

Nianze na nukuu hizi mbili kuntu za Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere- Mwenyezi Mungu amrehem...
Read More

Rais Magufuli Awataka Watanzania Waepuke Misaada ya Masharti Toka kwa Wazungu.....Pia ameahidi Kuwapunguzia Kodi Wafanyakazi Hadi Asilimia 10 au 9

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefika nyumbani kwake katika kijiji cha Mlimani, Wilaya ya Chato Mkoani Geita kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Rais, ambapo akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya sekondari Chato, ametoa wito kwa kila mtanzania kuchapa kazi kwa juhudi ili nchi iondokane na utegemezi wa misaada...
Read More

Global Catholic Network founder Mother Angelica has died

Associated Press 14 hours ago 

Penny azimia ndani ya gari, ala mzinga


Muonekano wa gari hilo baada ya kugongwa.
Stori:  Imelda Mtema, Wikienda
Dar es Salaam: Bidada yamemkuta! Mtangazaji wa Zuku TV, Penniel Mungilwa ‘VJ Penny’ amekumbwa na mkasa mwingine baada ya gari lake kupigwa mzinga maeneo ya Mikocheni jijini Dar, kwa kile kinachodaiwa alizimia barabarani kutokana na tatizo la ini linalomsumbua kwa sasa.
Chanzo makini ambacho kilishuhudia tukio hilo kilisema kuwa staa huyo alikuwa akiendesha gari lake aina ya Toyota Mark X kwa mwendo wa kawaida lakini akaanza kupunguza spidi taratatibu kutokana na maumivu yaliyompata ghafla na kusababisha bodaboda kugonga gari lake kwa nyuma.
peni2Mashuhuda wakiwa kwenye tukio.
Mpashaji wetu aliendelea kusema kuwa, wakati tukio hilo linatokea ilikuwa mchana kweupe bodaboda nusura wamfanyizie.
Pamoja na watu kusogelea kwenye tukio, Penny aliendelea kukaa ndani ya gari akiwa amejilaza hadi alipopata nafuu ndipo akaanza kuondoa gari taratibu.
Wikienda lilipozungumza na Penny alisema alipatwa na hali hiyo huku mwili ukiishiwa nguvu lakini kwa sasa yuko sawa.
pennyMtangazaji wa Zuku TV, Penniel Mungilwa ‘VJ Penny’.
Penny anakabiliwa na tatizo la kuharibika kwa ini kufuatia unywaji wa pombe kali kwa muda mrefu.
Hivi karibuni, Penny aliyekuwa mpenzi wa Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ aliripotiwa kuwa na tatizo la ini kutokana na unywaji wa pombe kali.

Wastara atoroshwa hospitalini

DSC_5306Staa wa Bongo Muvi, Wastara Juma akiwa hoi hospitali.
Stori:   Dustan Shekidele, Wikienda
Morogoro: Taarifa mbaya! Staa wa Bongo Muvi, Wastara Juma ambaye mapema wiki iliyopita alidai kupewa talaka la mumewe, Sadifa Khamis Juma, Mbunge wa Donge, Zanzibar, anadaiwa kutoroshwa hospitalini kisha kupelekwa hoteli ya mafichoni huku akiendelea na matibabu.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Wastara aliyekuwa amelazwa kwenye Hospitali ya Misheni ya St. Herry Health Center iliyopo mjini hapa, aliondolewa wodini hapa usiku mnene huku akiwa bado hali yake ya kiafya haijatengamaa tangu alipolazwa mapema wiki iliyopita akisumbuliwa na presha na kisukari na baadaye kupoteza fahamu.DSC_5305
Nesi akimuhudumia.
Wikienda lilifika hospitalini hapo Jumamosi iliyopita na kuthibitishiwa kuondolewa kwa msanii huyo na mtu aliyedai kuwa ni babu yake aliyetajwa kwa jina la Abdulaziz Babu.
Kwa mujibu wa mmoja wa wahudumu waliokuwa zamu walioomba hifadhi ya majina, jamaa huyo alidai kuwa Wastara aruhusiwe kwani alihofia usalama wake na kwamba sehemu aliyopanga kumpeleka ni salama zaidi.
Baada ya kunusa ‘ubuyu’ huo hospitalini hapo, Wikienda lilimsaka Wastara kujua mahali alipo na hali yake lakini jitihada hizo ziligonga mwamba kwa kuwa namba yake ya simu haikuwa hewani.
DSC_5304Alipotafutwa mtu huyo anayedai ni babu wa Wastara alifunguka: “Ni kweli nimemuondoa Wastara hapo hospitalini kwa sababu za kiusalama. Yupo hotelini lakini siwezi kukuelekeza ni sehemu gani kwa sababu ukiandika itajulikana na tatizo litakuwa palepale.”
Wastara alikumbwa na hali hiyo ikidaiwa ilitokana na mgogoro wa ndoa yake na Sadifa iliyofungwa hivi karibuni na kushindwa kudumu.

BREAKING NEWS:WANNE WAFARIKI NA 38 WAJERUHIWA KATIKA AJALI YA BASI MKOANI IRINGA

Harakati za kutoa miili ya marehemu zikiendelea

Watu wanne wamefariki papo hapo na wengine 38 wakijeruhiwa vibaya ikiwa ni pamoja na kukatika viungo, kufuatia ajali ya basi iliyotokea majira ya saa tano usiku wa leo mjini Iringa.
Basi hilo lenye namba za usajili T 798 AKV mali ya kampuni ya Lupondije Express lilikuwa likitokea mjini Mwanza kuelekea mjini Iringa.
Taarifa ambazo mwandishi wa habari hizi amezipata toka eneo la tukio, zinabainisha kuwa, chanzo cha ajali hiyo, ni kufeli kwa mfumo mzima wa breki, ambapo gari hilo likiwa katika mteremko mkali wa Ipogoro, lilimshinda dereva na kugonga kingo za barabara na hatimaye kuanguka.

20 Watiwa Mbaroni Wakituhumiwa Kumpiga Mawe Ofisa wa JWTZ Aliyemgonga Mtembea Kwa Miguu

Polisi mkoani Ruvuma inawashikilia waendesha bodaboda 20 Manispaa ya Songea wanaodaiwa kumshambulia askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Kikosi cha 411 KJ Ruhuwiko, kwa kupiga mawe gari alilokuwa akiendesha baada ya kumgonga mtembea kwa miguu. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Zubeir Mwombeji alisema tukio hilo lilitokea Machi 24 saa 3.00 usiku maeneo ya Shule ya Msingi Mfaranyaki,...
Read More

Ray c anaswa…

IMG-20160325-WA0002
Stori:  Musa Mateja, Wikienda

DAR ES SALAAM: LICHA ya kutumia nguvu nyingi kukanusha habari zinazochapishwa na Magazeti Pendwa ya Global Publishers kuwa, amerejea kwenye matumizi ya madawa ya kulevya ‘unga’, hatimaye staa wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ amenaswa ‘laivu’ akiwa ‘ameangusha gari’ kando ya barabara, habari ndiyo hiyo!
Ray C ambaye kila anapoandikwa na Magazeti ya Global kuhusu kurejea kwenye unga, amekuwa akimtupia shutuma Mkurugenzi wa Global, Eric Shigongo kwamba anamchafua, alinaswa na mapaparazi wetu hivi karibuni maeneo ya Mwananyamala Magengeni, Dar akiwa amezima yeye na mwanaume aliyekuwa naye hali iliyompa urahisi paparazi wetu kuwafotoa picha za kutosha.
ISHU ILIANZA JANUARI
Januari mwaka huu, gazeti hili liliripoti habari iliyokuwa na kichwa; CHIMBO LA UNGA LA RAY C LAGUNDULIKA.
Baada ya habari hiyo kutoka, Ray C aliikanusha kupitia ukurasa wake wa Instagram akisema:
“Seriously kwa kweli huwa naumia sanasana kuona binadamu mwenzangu anadiriki kuniharibia jina langu ili yeye apate kula! Hamjui mnaniathiri kiasi gani na hizi habari zenu! Hiyo habari yaani ni ujingaujinga tu umeunganishwa na picha yangu bila hata uoga mmeichukua kutoka kwenye page yangu ya Insta. Mnazitumia kunichafulia jina langu tena wakati ndiyo kwanza nahangaika kurudi kwenye kazi yangu.”
IMG-20160325-WA0000TV ANDAGRAUNDI IKAMSAPOTI
Kama hiyo haitoshi, kituo kimoja cha runinga cha muda mrefu nchini lakini bado kiko ‘andagraundi’ kilimpa nafasi Ray C akanushe habari ya Ijumaa Wikienda pasipo kujua gazeti hili lilijiridhisha kabla ya kuandika habari hiyo.
SHIGONGO ATAKA UKWELI
Baada ya Ray C kuyaponda Magazeti ya Global kwenye runinga kwa kudai yanamchafua, Shigongo alimuagiza Mhariri Kiongozi wa Magazeti Pendwa, Oscar Ndauka kupanga makachero kutokea kwenye kikosi maalum cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ ili kufuatilia nyendo za msanii huyo kama kweli anaonewa au la na kutaka matokeo yaliyo kamili!
OFM KAZINI
Timu ya OFM ilipangwa kwa zamu kumfuatilia Ray C kwa saa ishirini na nne ili kujiridhisha juu ya malalamiko yake, hasa kwamba Global inaungaunga picha za zamani ili kupata habari kama alivyosema kwenye Instagram yake.
Tangu Januari hiyo, timu ya OFM ilianza kuwa sambamba na Ray C huku makachero wengine wakiwasaka watu wake wa karibu ili kusikia chochote kutoka kwao.
MSIKIE HUYU
“Mimi ni miongoni mwa watumiaji wa madawa ya kulevya ambaye nilishawishiwa na Ray C kuacha na kunileta hapa kwenye Kituo cha Mwanayamala (hospitali) kwa ajili ya kuanza kumeza Methadone (dawa za kuponya waathirika wa madawa ya kulevya) ili niweze kurudia hali yangu ya kawaida. Hali yangu sasa niko safi na najitambua.
IMG-20160325-WA0001AMSIKITIKIA RAY C
“Kinachoniuma ni Ray C ambaye aliniunganisha hospitali kwa mbwembwe, yeye ameshindwa kuendelea na kapata bwana ambaye amemsaidia kurudia tena matumizi ya unga kushinda zamani. Huwezi amini kwa sasa mwenzetu gari limewaka upya, anawasumbua hata madaktari wetu, wakati mwingine wamekuwa wakishindwa kumhudumia.
FULL VURUGU
“Akija hapa kituoni kuchukua dawa muda wote ni kuwasimanga hawa wauguzi wetu jambo ambalo linatukera sana kwani anatuharibia hata sisi ambao alituleta. Aliyemponza ni Frank. Frank alikuja hapa kituoni kama mwathirika na kuanza kutumia dawa.
“Baada ya kukutana na Ray C na kuwa marafiki, wameshindwa kuendelea kutumia dawa. Badala yake wamekuwa wakivuta unga kiasi cha kuzima na kuleta fujo tu. Huyu Frank anaishi Mwananyamala karibu na hapa hospitali,” alisema mwathirika mmoja akiomba kufichiwa jina lake.
MADAKTARI WALIMSUSA
Akaendelea: “Unajua  madaktari wa hapa  walifikia hatua ya kujivua kumhudumia na kumrejesha kwao kipindi kile alipofanya fujo Posta. Ninasema haya kwa uchungu maana hata sisi tunaokunywa naye dawa hakuna hata mmoja anayeweza kummudu zaidi ya huyo Frank ambaye naye gari limeshachanganya, anampoteza kabisa Ray C,” kilisema chanzo hicho.”
JK ANYOOSHA MIKONO, AMUACHIA MAGUFULI
Chanzo kingine kilichopo kwenye hospitali hiyo kililiambia Ijumaa Wikienda kuwa, kutokana na JK kumsaidia alipokuwa madarakani na mrembo huyo kurejea tena kwenye unga, amenyoosha mikono, jukumu hilo litabaki kwa rais wa sasa, Dk. John Pombe Magufuli ‘JPM’.
IMG-20160325-WA0004“JK ameshanyoosha mikono. Hawezi tena kumuelewa huyu dada, amemuachia Magufuli naye labda ajaribu kwani ndiye aliyeko madarakani,” kilisema chanzo hicho.
RAY C MWENYEWE HUYU HAPA
Alipotafutwa Ray C juzi na kusomewa madai hayo na kuelezwa juu ya kupigwa picha zinazomuonesha akiwa amezima, alifunguka:
“Kweli kuna picha nimesikia watu walinipiga nikiwa nimezimika lakini siyo kwamba nilivuta unga kiasi hicho, picha hizo nilipigwa kweli nikiwa nimezima baada ya kunywa dawa hapo hospitali maana dawa ninazokunywa huwa ni kali sana, saa nyingine huwa nashindwa kujizuia na kujikuta nimezima.
“Kwanza unatakiwa ujue kwamba hizi dawa siku zote ukinywa hata kama ungekuwa na nguvu kiasi gani lazima kuna muda unafikia hatua ya kushindwa kabisa kujimudu na saa nyingine huwa tunalala hata na wenzangu kwani hata hizo picha wamenipiga chini ya mti hapahapa jirani na eneo la hospitali, siku hiyo nilikuwa nimezidiwa sana.”
AMTAJA FRANK KAMA ‘BEBI’ WAKE
“Ninachokijua nilala chini ya mti na Frank lakini hata ukiangalia nyuma yetu pia
kuna watu kibao ambao nao walikuwa wamelala baada ya kunywa dawa na kuzidiwa, sasa sijui wewe hizo zangu na huyo mpenzi wangu umezitoa wapi,” alisema Ray C.
DAKTARI WA WAATHIRIKA AZUNGUMZA
Baada ya utetezi huo wa Ray C, gazeti hili lilimwendea hewani daktari wa tiba kwa waathirika na unga kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (jina lipo) na kumuuliza kama matumizi ya dawa za Methadone yanaweza kumzimisha mtumiaji ambapo alisema:
“Kama anayetumia Methadone baada ya kuathirika hatatumia madawa ya kulevya hawezi kuzima kwa namna yoyote ile. Ukimwona mtu anazima ujue anachanganya, yaani anameza Methadone pia anaendelea kubwia unga.”
TUMEFIKAJE HAPA?
Ray C aliyewahi kutamba na nyimbo nyingi kali, ikiwemo Na Wewe Milele, alijikuta ametopea kwenye madawa ya kulevya baada ya kutumbukia kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa staa wa Hip Hop Bongo, Isaac Waziri Makuto ‘Lord Eyez’ ambaye naye anadaiwa kutumia.
Baadaye wawili hao walimwagana huku Ray C akichanja mbuga katika eneo hilo hali iliyomlazimisha ‘kustaafu’ muziki kutokana na mwili kukosa mawasiliano katika kupanga mikakati.
Gazeti damu moja na hili, Ijumaa, toleo Namba 799 la Novemba 2-8, 2012 lilitoa picha za Ray C akiwa amezimika na habari yenye kichwa; DAH!
RAY C. Tukio hilo lilijiri maeneo ya Magomeni, Dar.
JK ASOMA, APATA UCHUNGU
Wiki moja baada ya gazeti hilo kuingia mtaani likielezea hali ya Ray C, JK alimwita Ikulu ya Dar es Salaam yeye, mama yake mzazi, Margaret Mtweve na ndugu mwingine hali iliyoonesha kuwa, aliisoma habari hiyo kwenye Gazeti la Ijumaa.
Lengo la kumwita lilikuwa kumsaidia mwanamuziki huyo kwa tiba na uangalizi wa kina jambo ambalo lilifanyika na akarudia kwenye hali yake ya kawaida.
Mwaka 2015, baada ya minong’ono mingi kwamba msanii huyo amerejea katika matumizi ya unga, magazeti ya Global yaliandika habari hiyo na Ray C akawa anakanusha mara kwa mara mpaka majuzi aliponaswa akiwa amezima.

Hofu ya kutemwa? DC amtishia mwandishi wa habari: "umeamua kutumaliza, tutamalizana…"

3/26/2016 06:16:00 PM
Karen Yunus
Karen Yunus
Mkuu wa Wilaya ya Magu, Karen Yunus amemtolea maneno ya vitisho mwandishi Neema Emmanuel na kumhoji iwapo kuna mtu anamtuma kutokana na kile alichodai kuwa ni mwandishi huyo kumchafua kwa namna anavyong’ang’ania kuripoti hali mbaya ya Shule ya Msingi Lupemba iliyopo wilayani kwake.

Shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2006 na kuwa na wanafunzi 651, ilifungwa kwa muda usiojulikana mapema mwaka huu ili kupisha ujenzi wa vyumba walau vinne vya madarasa. 

Nipashe iliripoti Jumapili iliyopita (Machi 20) kuwa uamuzi wa kuifunga shule hiyo ulitolewa Februari 8, ikiwa ni siku moja tu baada ya gazeti hili kuripoti changamoto mbalimbali zinazokwaza maendeleo ya shule hiyo.

Taarifa ya Nipashe ilikua siku mbili tu baada ya Rais John Magufuli kueleza katika maadhimisho ya kilele cha miaka 39 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Singida kuwa wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa mikoa watakosa sifa katika serikali yake ikiwa kwenye maeneo yao kutakuwa na wanafunzi wanaoketi chini kwa kukosa madawati.

Aidha, Nipashe ilieleza katika habari hiyo ya Jumapili iliyopita (Wanafunzi wachunga ng’ombe Magu wakisubiri madarasa kujengwa), kuwa baada ya kufungwa kwa shule ya Lupemba huku wanaoendelea na masomo wakiwa ni wanafunzi wa madarasa ya nne na saba peke yake, baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakijihusisha na shughuli nyingine zisizokuwa za masomo nyumbani kwao ikiwa ni pamoja na kuchunga ng’ombe.

Baada ya kuchapishwa kwa habari hiyo, DC Karen alimpigia simu mwandishi na kumpa vitisho kutokana na kile alichodai kuwa hajamtendea haki. DC Karen alipiga simu hiyo Jumapili iliyopita, majira ya subuhi.

“Haya mambo unayoyafanya siyo mazuri kwa sababu tunajitahidi… lakini wewe unaendelea kutuchafua tu, hujatenda haki,” alisema DC Karen katika moja ya matamshi yake kwa mwa mwandishi na kuongeza: 

“…kwa sabababu haya mambo unayoyaandika yanasomwa na wengine ambao wana maamuzi makubwa… wee unatumwa nini? Kuna mtu anakutuma? Na kama hakuna mtu anakutuma kwa nini unang’ang’ania hivyo?”

Aidha, katika vitisho vyake hivyo kwa mwandishi, DC Karen aliyehamishiwa Wilaya ya Magu akitokea Sengerema kutokana na mabadiliko aliyoyafanya Rais Jakaya Kikwete Februari mwaka jana, alimuonya mwandishi kwa kumuelezea kuwa ni mtoto mdogo anayelingana na mtoto wake wa mwisho na kwamba, kitendo chake cha kuripoti suala la Shule ya Lupemba bila ‘kubalance’ ni sawa na kutaka kuwamaliza na hivyo ajue kuwa "tutamalizana".

“Mi nakwambia... halafu wee bado mtoto mdogo… wee una miaka mingapi… wewe ni mwanangu wa mwisho… mi nakwambia Neema… lakini kwa sababu umeamua kutumaliza, tutamalizana… lakini na wewe you should wait for your chance (usuburi nafai yako), na hayo mambo yapo nakwambia," alisema DC Karen katika baadhi ya vitisho alivyotoa kwa mwandishi.

"Andika neno karma… usipende kuharibia watu wanajihangaikia maisha yao, kwa miaka mingi, eeh.”

Kwa mujibu wa kamusi ya Kiingereza ya Oxford, neno ‘karma’ lina asili ya Kibudha na Kihindi na maana yake ni malipo anayoweza kuyapata mtu kutokana na matendo yake; kwamba akitenda ubaya hulipwa ubaya na akitenda mema atalipwa kwa wema wake.

UKWELI KUHUSU SHULE YA LUPEMBA

Nipashe imekuwa ikiripoti mfululizo wa taarifa kuhusiana na ukosefu wa miundombinu na changamoto mbalimbali zinazoikabili shule hiyo ya Lupemba yenye wanafunzi 651, na ambayo ilijengwa mwaka 2006.

Kwa mara ya kwanza, Nipashe iliripoti taarifa hiyo Jumapili ya Februari 7, 2016 huku ikiwa na kichwa cha habari ‘Elimu ya bure mtihani mzito’, pamoja na picha ya ukurasa wa mbele inayoonyesha baadhi ya wanafunzi wakiwa wamekalia vitofali katika mojawapo ya banda la miti na nyasi lililokuwa likitumiwa kama darasa. 

Wiki iliyopita, Nipashe iliripoti tena juu ya shule hiyo, kwa kueleza athari zitokanazo na uamuzi wa Feberuari 8, wa uongozi wa wilaya ambao ni kuifunga kwa muda usiojulikana ili kupisha ujenzi wa vyumba vya madarasa walau vinne na kwa ujumla kuboresha mazingira ya upatikanaji wa elimu shuleni hapo. 

Aidha, katika taarifa hiyo, zilioenekana picha za wanafunzi wa shule ya Lupemba wanaolazimika kusaidia wazazi wao shughuli za kila siku ikiwamo kuchunga ng’ombe baada ya shule yao kufungwa kwa muda usiojulikana.

Katika tarifa hiyo, mwandishi alikutana na wanafunzi kadhaa na kuzungumza nao ambapo walielzea masikitiko kutokana na uamuzi wa kufungwa kwa shule yao na wao kurudishwa nyumbani badala ya kuhamishiwa walau kwa muda katika shule nyingine.

Aidha, mwandishi alizungumza pia na wazazi wakiwamo Mathias Musuka na Salome Makoye, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Lupemba, Daniel Matemi; mwalimu wa kawaida, Johannes Rutaihwa; Kaimu Afisa Elimu ya Msingi wilayani Magu, Veronica Justine; Mkurugenzi Msaidizi wa Udhibiti wa Ubora wa Shule Wilaya ya Magu, Joseph Kaswa; Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Ntinika Paul ; aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo na pia yeye mwenyewe, Mkuu wa Wilaya ya Magu - Karen Yunus.

“Ni kweli nimepata vitisho kutoka kwa Mkuu wa Wilaya… lakini sioni nilichokosea kwa sababu hakuna lisilokuwa la kweli katika ripoti hiyo,” alisema mwandishi Neema wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii kuelezea vitisho alivyopata kuhusiana na ripoti juu ya hali ya shule ya msingi Lupemba. 

"Shule imefungwa na wanaosoma ni madarasa ya nne na saba, kuna watoto hivi sasa huishia kuchunga ng’ombe. Yote hayo ni kweli tupu."

Je, hivi sasa hali katika shule hiyo ya Lupemba ikoje? Usikose kufuatilia mwenendo wa ripoti maalum kuhusu shule hiyo katika gazeti hili kesho).

BREAKING NEWS: BASI LA MACHAME LAPINDUKA ENEO LA MSATA MKOANI PWANI

 Watu wawili wamejeruhiwa na wengine kadhaa kunuaurika baada ya basi walilokuwa wakisafiria kupinduka katika eneo la Msata, mkoani Pwani.
Taarifa kutoka eneo la tukio zinasema kuwa waliojeruhiwa ni pamoja na dereva wa basi hilo, mali ya kampuni ya Machame, lenye namba za usajili T 712 DCL.
Basi hilo lililokuwa linatoka Dar kuelekea Arusha, lilipinduka kufuatia kupasuka kwa tairi ya mbele upande wa kulia, ambapo liliacha njia na kugonga kingo za barabara. Mwingine ni mwanamke ambaye jina lake pia halijaweza kupatikana, ambaye alikuwa abiria katika basi hilo.

Kichupa cha leo UDZM QS BAND -Nishukie wapi? (Official video)

Kenya Embassy to Hold Event for Kenyan ID/Passport Renewal and Dual Citizenship Applications in Jersey City, NJ on April 2nd & 3rd, 2016

By Mwakilishi 

The Embassy of the Republic of Kenya in Washington, DC will be holding a Kenyan National ID/PassportEvent in Jersey City, New Jersey on Saturday, April 2nd, 2016 and Sunday, April 3rd, 2016.
The following services will be provided:
Application of Kenyan National ID
Application of new and Renewal of Kenyan Passport
Application for Dual Citizenship
The Embassy require that you bring your completed applications, required supporting documentsmoney order and self-addressed envelopes as outlined at the Embassy websitewww.kenyaembassy.com/id.html
The events will take place as follows:
Saturday, April 2nd from 3pm to 9pm
St Patrick’s Church
492 Bramhall Ave, Jersey City, NJ 07304
Sunday, April 3rd from 2pm to 4pm
Kingdom Ambassadors Church
91 Jefferson Blvd, Edison, NJ 08817
For more informationcontact:
Dr David Angwenyi: 609-429-0529
Zachary Moitui: 201-889-3636
Nelly Nzisa: 908-331-1961
Maria Kioko: 201-320-3048
Faith Maina: 201-920-7621
Mary Muturi: 908-416-0281
Pastors Dominic & Carol Macharia: 732-986-6524
  • National science teachers association
  •  
  • Renewal