MAJALIWA AITEMBELEA FAMILIA YA MAREHEMU SITTA


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mama Margart Sitta, mjane wa Spika mstaafu,  Sumuel Sitta wakati alipoitembelea familia ya marehemu jijini Dar es salaam Desemba 19, 2016. Kulia ni mkewe Mary. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
   Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (kushoto  kwake) wakiwa katika picha ya pamoja na familia ya aliyekuwa Spika Mstaafu, Samuel Sitta wakati walipoitembelea familia hiyo, nyumbani kwa marehemu jijini Dar es salaam Desemba 19, 2016. Kulia kwake ni mjane wa marehemu, Margareth Sitta. Wengine pichani kutoka kushoto ni watoto wa marehemu, Benjamin Sitta, John Sitta na Sam Junior.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  na mkewe Mary wakisalimiana na mama Margaret Sitta, mjane wa alieyekuwa Spika mstaafu, Samuel Sitta wakati walipoitembelea familia ya Spika huyo jijini Dar es salaam Desemba 19, 2016. Wengine pichani ni watoto wa marehemu, kutoka kushoto ni  Benjamin Sitta, Sam Junior na John Sitta. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

JESHI LA POLISI LAMTIA MBARONI MTUHUMIWA WA UTAPELI


Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Kamishna Msaidi wa Polisi (ACP), Advera  Bulimba

Na Dotto Mwaibale
JESHI la Polisi nchini limefanikiwa  kumkamata mtuhumiwa wa utapeli anayejulikana kwa jina la  Wilfred Masawe (36) , Kabila mchaga na  mkazi wa  Buza, Temeke jijini Dar es Salaam.

Akitoa taarifa hiyo kwa vyombo vya habari Dar es Salaam leo, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Kamishna Msaidi wa Polisi (ACP), Advera  Bulimba amesema  mtuhumiwa huyo alikuwa akitumia mbinu mbalimbali kutapeli zikiwemo kujitambulisha kama kiongozi wa serikali kwa kutumia mtandao wa Whatsapp,  huku akieleza kuwa yupo nje ya nchi na kuna tatizo la msiba ambao umetokea nchini na unamuhusu na hivyo alikua akitoa maelekezo kwa watendaji wa serikali waweze kusaidia gharama za matibabu hospitalini, gharama za kusafirisha mwili wa marehemu na gharama za mazishi.

Alisema pia alikuwa akitumia mbinu ya kujifanya kiongozi mkubwa wa dini ya kikristo (Askofu) na kuwaambia waumini na viongozi mbalimbali kuhusu maandalizi ya makongamano ya kidini kwa lengo la kuwaomba michango kuweza kufanikisha makongamano hayo.

Vodacom, WCB waja na Tamasha la ‘Nogesha Upendo’

003-nogesha-upendo

Baadhi ya wasanii wa nembo ya WCB wakiongozwa na Diamond Platinumz wakiwasili katika makao makuu ya Vodacom Tanzania, yaliyopo Mlimani City jijini Dar es Salaam katika mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na tamasha la “Nogesha Upendo” litakalofanyika Desemba 24 katika fukwe za Jangwani Sea Breeze jijini Dar es Salaam na Desemba 25 Iringa katika Uwanja wa Samora chini ya udhamini wa Vodacom Tanzania.
001-nogesha-upendo
Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Nandi Mwiyomella (kushoto) akimsikiliza Msanii wa muziki wa kizazi kipya wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz (kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya kutanga tamasha la “Nogesha Upendo” yatakayofanyika Desemba 24 katika fukwe za Jangwani Sea Breeze jijini Dar es Salaam na Desemba 25 Iringa katika uwanja wa Samora chini ya udhamini wa Vodacom Tanzania.
002-nogesha-upendo
Msanii wa muziki wa kizazi kipya wa Bongo Fleva, Diamond Platinumz (katikati) akipiga selfie na baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania mara baada ya mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na tamasha la “Nogesha Upendo” litakalofanyika Desemba 24 katika fukwe za Jangwani Sea Breeze jijini Dar es Salaam na Desemba 25 Iringa katika Uwanja wa Samora chini ya udhamini wa Vodacom Tanzania.
DAR ES SALAAM: Katika mwendelezo wake wa kuwapatia wateja wake na Watanzania wote kwa ujumla burudani za sikukuu, Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na wasanii wa WCB imeandaa matamasha mawili ya kukata na shoka ambayo yatafanyika katika msimu huu wa sikukuu.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa kampuni hiyo, Nandi Mwiyomella, alisema matamasha hayo makubwa ya muziki wa kizazi kipya yatafanyika katika mikoa ya Dar e salaam na Iringa chini ya wasanii Diamond Platinumz, Rayvanny , Rich Mavoko, Harmonize na Queen Darleen.
“Kama mnavyoelewa msimu huu huwa umeambatana na shamrashamra mbalimbali za sikukuu na mitoko ukiwa na familia yako, Desemba 24 kutashushwa shoo ya Nguvu katika fukwe za Jangwani Sea Breeze Hotel ambapo kutakuwa na tamasha la kihistoria la “Vodacom Wasafi Beach Party” na Iringa tamasha litafanyika siku ya Krismasi katika uwanja wa Samora na Matamasha yote yataanza saa nane mchana”.Alisema.
Mwiyombella alisema burudani hii ya muziki inakwenda sambamba na promosheni ya Nogesha Upendo ya http://vda.cm/nogeshaupendoVodacom inayolenga kuwapatia wateja wote wa mtandao wa Vodacom zawadi za sikukuu ikiwa ni shukrani kwa wateja ambapo pia wateja wanayo fursa ya kujishindia tiketi za bure za kushiriki katika matamasha haya makubwa katika msimu huu wa sikukuu.

“Ili kujishindia tiketi ya bure anachotakiwa kufanya mteja wa Vodacom ni kupiga *149*01# kisha nunua kifurushi chochote cha Vodacom na moja kwa moja utakua umeingia katika droo ya kuweza kujishindia tiketi yako. Zawadi nyingine kemkem kupitia promosheni ya Nogesha Upendo ni fedha taslimu, muda wa maongezi, Vifurushi vya intaneti (Mb).” Alisema.
Naye Msanii wa muziki wa kizazi kipya anayetamba katika anga za kimataifa, Diamond Platinumz akiongea kwa niaba ya wasanii wa WCB alitoa wito kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na Iringa kujitokeza kwa wingi siku ya shoo hizo kwani zitakuwa ni shoo za kihistoria katika mikoa hii miwili kufanywa na Vodacom kwa kushirikiana na WCB, Napenda kuwahakikishia mashabiki wetu kwamba tutakamua vilivyo tukiwa na wasanii wenzangu wote wa WBC kwa “Kunogesha Upendo” Alisisitiza Diamond.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya Disemba 17

NDUGU YETU FIDELIS MALOKO ANAOMBA MSAADA WAKO

Ndugu zangu Watanzania wenzangu poleni na majukumu, Mtanzania mwenzetu, ndugu yetu, rafiki yetu na jirani yetu Fidelis Maloko anaeishi Durham, North Carolina anaumwa sana figo zote hazifanyi kazi sasa hivi anatumia mashine, hali yake kusema ukweli ni mbaya na sasa hawezi kufanyakazi tena, pesa yake ya akiba imemalizika kwenye matibabu na dawa.

Huyu Fedelis Maloko ni ndugu yetu, Mtanzania mwenzetu anateseka sana, kama tujuavyo maisha hayatabiriki, mimi na wewe hatujui nini kitatokea kesho na ndugu yetu Fidelis Maloko hakuchagua hali hii aliyokuanayo, ni mipango ya mwenyezi Mungu juu yake.

Naomba kama umeguswa tafadhali msaidie ndugu yetu, mtanzania mwenzako wewe ndiye ngugu yake wa karibu hapa ughaibuni.

Chochote ulichonacho kitabadilisha maisha ya Fidelis Maloko, kwa niaba ya Fidelis Maloko natanguliza shukurani mno kwa mchango wako.

Pope's choir spreads message of harmony in music

CBS News 

Owner With Obstructing Police

VOA News 

MWANZILISHI WA JAMIIFORUMS AFIKISHWA MAHAKAMANI, AKOSA DHAMANA

Mwanazilishi wa Mtandao wa JamiiForums aliyekamatwa na Polisi kuanzia juzi Maxence Melo, leo amefikishwa mahakamani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisitu Jijini Dar es Salaam leo asubuhi na kusomewa mashtaka matatu.

Melo amefikishwa mahakamani leo ikiwa ni baada ya sitofahamu kubwa iliyokuwa imetanda kuhusu kosa hasa la kukamatwa kwake ambapo tangu alipokuwa amekamatwa zaidi ya saa 24 zilizopita hakuwa amefikishwa mahakamani huku Polisi wakiwa wamefanya upekuzi ofisini kwake na nyumbani.

Maxence Melo amepandishwa kizimbani leo na kusomewa mashtaka matatu yanayomkabili likiwemo la kumiliki na kuendesha tovuti ambayo haijasajiliwa hapa nchini Tanzania (JamiiForums).

Mahafali ya 14 ya Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA) yafana, jijini Dar

Kikosi cha brasband cha Magereza kikiongoza Maandamao kuelekea uwanjani kwenye mahafali ya 14 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kwa Kampasi ya Dar es salaam na Mtwara leo jijini Dar es Salaam.Walioko nyuma ni baadhi ya wahadhiri wa Taasisi ya  Uhasibu Tanzania (TIA). ( Picha na Geofrey Adroph)
Mgeni Rasmi Naibu Gavana wa Benki Kuu Dkt. Natu A. Mwamba(katikati) akiongoza maandamano ya mahafali ya 14 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kwa Kampasi ya Dar es salaam na Mtwara leo jijini Dar es salaam. Wa kwanza kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania Dk. Joseph Kihanda.

Death Announcement: Geofrey Riri (Big Jofu) of Grandview, MO

Posted by  

big-jofu
Print Friendly
We regret to announce the sudden death of Geofrey Riri, husband to Annette Riri of Grandview, MO.
He was the father of four: Davida (5), Simeon (6), Virginia (13), and Zakayo (14).   He passed away on 12/13/2016 of an apparent heart attack.
Currently family and friends are meeting every day at his home in Grandview.  Further funeral arrangements will be communicated as it gets confirmed.  Every support is welcome and appreciated.
You can contribute towards his funeral expenses by clicking here https://www.gofundme.com/geofrey-big-jofu-riris-memorial

Kenyan man Biko Wambugu Wachira nephew to Mike Wambugu of Dallas, TX killed in car accident in Columbus Ohio

Posted by  

biko-wachira
Print Friendly
A Kenyan man was killed in a single-vehicle crash in Columbus, OH on Saturday.
40-year-old Biko Wambugu Wachira was killed after his vehicle veered off the road and hit a concrete wall.
Wachira’s vehicle then went across the freeway, crashing into guardrail and into the median. The accident happened on SR315 in the area of the Bethel Road overpass about 3:30 a.m.
He was declared dead at the scene of the accident.
The cause of the deadly crash had not been determined at the time of the report.
The police are still investigating the cause of the crash site and hope to learn the cause of the incident as the investigation concludes.
Mr Wachira is a nephew to Mike Wambugu of Dallas, TX.
wachira2wachira3wachira4

Kenyatta National Hospital Shut Down Indefinitely after Doctors Join Strike

Posted by  

knh
Print Friendly
Kenyatta National Hospital will no longer be operational until a strike impasse is resolved.
Approximately 300 doctors and consultants from both KNH and the University of Nairobi (UoN) Wednesday downed their tools until all their demands are met by the Government.
 “No patient should be referred to Kenyatta because the doctors have now joined the strike. We had tried offering the basic services hoping that the issue would be addressed in due time but the Government still hasn’t signed the CBA,” said a professor from the UoN Department of Medicine.
The health workers came to the conclusion after a meeting Wednesday morning.
The country’s largest referral hospital had been operational despite the industrial action.
But the doctors and consultants called it quits after the Government took a hard-line stance on fulfilling their demands, which included signing the 2013 Collective Bargaining Agreement (CBA).
Downing of tools
The doctors said the downing of tools would affect both the public and private wings as well as the inpatient and outpatient departments.
Kenya Medical Practitioners, Pharmacists and Dentists Union Secretary General Ouma Oluga maintained the only way doctors would resume work was if the State signed the 2013 deal.
He also called for the withdrawal of the Kenya Defence Forces (KDF) that had been stationed at the facility’s casualty wing.
“I have been receiving calls from our KDF colleagues who say that they are fatigued and not qualified to handle such cases. Thus I recommend that they are deployed back to the army base,” suggested Oluga.
The secretary general further accused the state of running away from the doctors’ problem, saying they were not afraid of going to jail if it was the only way to access justice. Oluga said doctors could barely afford access to medical services.
Meanwhile, approximately 20 people have died as a result of the impasse between the two bodies, with others seeking treatment outside Kenya.
-standardmedia.co.ke

Aunt Ezekiel: Kama Nina Mimba, Hairudi Ndani, Itatoka Nje (+Video)


Aunt Ezekiel: Kama Nina Mimba, Hairudi Ndani, Itatoka Nje

Waziri Mkuu Acharuka....Asema NGO Chonganishi Zitafutwa

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa miezi sita ya kujitathimini mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) yanayofanya kazi zake wilayani Ngorongoro mkoani Arusha, kama yanafanya kazi kwa misingi ya sheria na maadili. Baadaye, yatahakikiwa na kama yatabainika yanachochea migogoro, yatafutwa. Pia, Majaliwa amezicharukia NGOs nyingine zinazoitangaza vibaya Tanzania kimataifa kwa kupiga picha za...
Read More

Waziri Mkuu Amsimamisha Kazi Mwekahazina Wa Wilaya Ya Bahi.......Aagiza arudishwe Longido kujibu tuhuma zinazomkabili

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi aliyekuwa Mwekahazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido, Bw. Issai Mbilu ambaye kwa sasa amehamishiwa Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma na kuagiza arudishwe haraka na kuja kujibu tuhuma za ubadhilifu sh. milioni 642.4 za miradi zinazomkabili. “Tunaendelea kudhibiti na kuweka nidhamu ndani ya Serikali. Ukiharibu Longido usitegemee kuhamishiwa wilaya...
Read More

Have a spirit of Excellence - Joel Osteen


IOP WAMEMA NDOA ZA UTOTONI ZINAZIDI KUONGEZEKA MKOANI IRINGA

 hawa ni baadhi ya wananchi wa kabila la kimasai ambalo linakaliwa na tuhuma za kuozesha wasicha wenye umri mdogo.
hili ni jengo la shirika lisilo la kiserikali la Ilula Ophan program (IOP)

na Fredy Mgunda,Iringa
Shirika lisilo la kiserikali la Ilula Ophan program (IOP) limeendelea kukemea na kutoa elimu juu ya ndoa za utotoni kwa kuwa zinarudisha maendeleo nyuma ya wasichana wa jamii ya kimasai.

Akizungumza na blog hii Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Ilula Ophan program (IOP) Edson Msigwa alisema kuwa tatizo la ndoa za utotoni katika kabila la wamasai bado ni kubwa.

Msigwa alieleza jinsi gani wanavyofanya shughuli za kukemea na kutoa elimu juu ya ndoa za utotoni katika jamii ya wamasai