MWANZILISHI WA JAMIIFORUMS AFIKISHWA MAHAKAMANI, AKOSA DHAMANA

Mwanazilishi wa Mtandao wa JamiiForums aliyekamatwa na Polisi kuanzia juzi Maxence Melo, leo amefikishwa mahakamani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisitu Jijini Dar es Salaam leo asubuhi na kusomewa mashtaka matatu.

Melo amefikishwa mahakamani leo ikiwa ni baada ya sitofahamu kubwa iliyokuwa imetanda kuhusu kosa hasa la kukamatwa kwake ambapo tangu alipokuwa amekamatwa zaidi ya saa 24 zilizopita hakuwa amefikishwa mahakamani huku Polisi wakiwa wamefanya upekuzi ofisini kwake na nyumbani.

Maxence Melo amepandishwa kizimbani leo na kusomewa mashtaka matatu yanayomkabili likiwemo la kumiliki na kuendesha tovuti ambayo haijasajiliwa hapa nchini Tanzania (JamiiForums).

No comments:

Post a Comment