Mwigulu ‘aisaidia’ polisi kukamata mtuhumiwa

Raia wa China, Leo Swi akikamatwa kwa tuhuma za
By Rehema Matowo, Mwananchi rmatowo@mwananchi.co.tz

Geita. Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ‘amelisaidia’ jeshi lake la polisi alipoongoza operesheni ya kumkata raia wa China anayedaiwa kumpiga mchimbaji mdogo na kumjeruhi katika mgodi wa dhahabu wa Nyamahuna uliopo wilayani Geita.

Tukio la kijana huyo kupigwa, lilisambaa kwenye mitandao ya kijamii mwishoni mwa wiki iliyopita ikidaiwa kuwa kijana huyo amepigwa hadi kuuawa baada ya kudai kuongezewa mshahara.

Taarifa hizo zilimlazimu Nchemba kufunga safari hadi katika Gereza la Geita na kukutana na kijana huyo, Masanja Shokala na kisha kuondoka naye akiwa amefungwa pingu hadi kwenye mgodi huo ili kuwatambua waliomtesa na kumpiga.

No comments:

Post a Comment