Walimu hawana ofisi, wafanya kazi chini ya mkorosho

SHULE ya Msingi Vikawe iliyopo Kata ya Pangani wilayani Kibaha mkoani Pwani inakabiliwa na changamoto ukiwemo upungufu wa matundu ya vyoo, madarasa na ofisi ya walimu na hivyo kufanya shule kutokuwa na mazingira rafiki ya utoleaji elimu.

Aidha wanafunzi wengi wanalazimika kujisaidia vichakani kutokana na upungufu wa matundu.

Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea shule hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Shule, Albert Nsajigwa amesema hata walimu hufanya kazi zao wakiwa chini ya mti.

Nsajigwa amesema walimu hao wamekuwa wakifanya majukumu yao chini ya mkorosho na kujiuliza hali inakuwaje inaponyesha mvua ilihali shule hiyo ikiwa na madarasa saba na kati ya hayo mawili yanatakiwa kuvunjwa kutokana na uchakavu.

"Tunaomba wadau watusaidie kwani hali ni mbaya sana miundombinu si rafiki kwa wanafunzi hata walimu na tulipeleka maombi yetu halmashauri kwa ajili ya kutusaidia lakini inaonekana mambo hayajawa mazuri na tukaona bora tuanze ujenzi wa vyoo vinne kwa nguvu ya wananchi," amesema Nsajigwa.

No comments:

Post a Comment