Kesi ya Mke wa Bilonea Msuya Yaahirishwa Tena


DAR ES SALAAM: MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu inatarajiwa kutoa uamuzi wa kumwachia  ama kutomwachia huru mke wa marehemu bilionea Erasto Msuya aitwaye Miriam Mrita (41) na mwenzake ambaye ni mfanyabiashara, Revocatus  Muyela (40), wanaotetewa na mawakili Peter Kibatala na John Mallya  ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Januari 23 mwaka huu.

Uamuzi huo ulitolewa leo mahakamani hapo kutokana na upande wa serikali kushindwa kubadilisha hati ya mashtaka ya kesi hiyo ndani ya siku mbili kama ilivyoamliwa Januari 9, mwaka huu.
 Januari 9, 2017 Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa, aliuamuru upande wa serikali kubadilisha hati ya mashitaka ndani ya siku mbili ambapo   alisema uamuzi huo  unatokana na kupitia hoja za pande zote mbili na kubaini kuwa hati ya mashitaka ilikuwa na mapungufu mawili likiwemo la kutoonyesha kama kuna mtu ambaye amesababisha kifo kwa mtu mwingine.

No comments:

Post a Comment