Magufuli, Museveni wagomea EPA

RAIS John Magufuli na mgeni wake Rais wa Uganda, Yoweri Museveni wamekubaliana kuhakikisha wanatumia fursa zilizopo kuongeza biashara kati ya nchi hizo ili kukuza uchumi wa nchi hizo mbili. Rais Museveni yupo nchini kwa ziara ya kiserikali ya siku mbili, ambapo jana alikuwa na mazungumzo ya kina na Rais Magufuli.
Akizungumza na waandishi wa habari, Rais Magufuli alibainisha kuwa mazungumzo yao pia yalilenga suala la kusaini Mkataba wa Ushirikiano wa Kibiashara (EPA) na nchi za Jumuia ya Ulaya (EU).
Rais Magufuli alisisitiza kuwa Tanzania haitasaini mkataba wa EPA na kubainisha kuwa hiyo ni njia nyingine ya ukoloni.
“Tumezungumza kwa kina na Rais Museveni na tumekubaliana kuendelea kulizungumza. Nimemueleza kuwa sisi Tanzania tunaona EPA haina faida na ni ukoloni mwingine, ambao unaletwa kwa sababu ya mambo mengi.
“Hatuwezi kuzungumzia kujenga viwanda wakati huohuo tunashindana na watu wenye viwanda vikubwa.
“Hili tumelizungumza kwa kina na tumekubaliana na Rais Museveni na jopo la wataalamu litakwenda Uganda Machi 18, kutoa maelezo ya kina. Na yeye Rais Museveni amesema kimsingi anapenda kufanya kitu chenye faida.” Rais Magufuli aliongeza:

No comments:

Post a Comment