Halmashauri zatisha kwa vyeti feki

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki
WAKATI Serikali imetangaza orodha ya majina ya watumishi wa umma wenye vyeti feki, Halmashauri za Miji, Wilaya, Manispaa na Majiji zimeongoza kwa kuwa na wafanyakazi wenye vyeti bandia huku taasisi za umma zikifuatia.

Hatua hiyo imekuja siku moja baada ya Rais John Magufuli juzi kupokea vitabu vyenye orodha ya watumishi wa umma ambao wamebainika kuwa ama na vyeti pungufu, vyeti tata na vyeti vya kughushi kutoka kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki.

Hatua ya kufanyika kwa uhakiki huo ambayo ilitokana na agizo la Rais Magufuli inafanya sasa kuwepo kwa nafasi wazi za ajira 12,000 kwa watu wenye sifa ambao wangeweza kuajiriwa katika nafasi hizo lakini nafasi zao zikakosekana kutokana na kuajiriwa kwa watu wasio na sifa.

No comments:

Post a Comment