SII MARA YA KWANZA KWA MGONJWA KUJIRUSHA GHOROFANI MUHIMBILI

By Herieth Makwetta, Mwananchi hmakweta@mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Katika hali isiyokuwa ya kawaida mgonjwa mmoja aliyekuwa amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alijirusha kutoka ghorofani jana asubuhi na kujeruhiwa kichwani.

Tukio kama hilo liliwahi kutokea mwaka 2012, katika wodi hiyo hiyo na dirisha hilo hilo.

Mgonjwa huyo (jina linahifadhiwa) alikuwa amelazwa wodi 6 katika jengo la Mwaisela.

Shuhuda wa tukio hilo Juma Omary alisema mgonjwa huyo alikuwa akiweweseka, kabla ya kuamka kitandani na kuanza kukimbia.

No comments:

Post a Comment