WAKAZI WA OLASITI JIJINI ARUSHA WASUSIA MAJI WASEMA HAYANA LADHA ,HAYAFAI KWA MATUMIZI YEYOTE

Baadhi ya wananchi wa Kata ya Olasiti kama wanavyoonekana  pichani.Picha na Vero Ignatus blog.

Na .Vero Ignatus,Arusha.
WAKAZI wa Olasiti jijini Arusha wamesusia maji yanayotolewa na Idara ya maji na kudai kuwa maji hayo hayafai kwa matumizi ya aina yoyote.

Wakizungumza  katika mkutano wa hadhara uliofanywa na mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo wananchi hao walisema maji yaliyosambazwa na Idara ya maji yana  chumvi kiasi cha kuharibu  hata mimea wanapojaribu kumwagilia.

Mmoja wa wakazi hao Meck  Mollel alisema wanahofia baada ya miaka ijayo kutokuwa na nguvu za kiume kutokana na kuendelea kutumia maji hayo ambayo yanaladha ya magadi.

"Kweli haya maji yanatupa hofu baadaye tutajikuta wanawake wote kwa mpango huu hatuyahitaji haya maji tuleteeni maji yaliyorafiki kwa binadamu" alisema Mollel.

No comments:

Post a Comment