KIKWETE AWATETEA WAPINZANI, ATAKA WASICHUKULIWE KAMA MAADUI

Rais mstaafu wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amevitaka vyama tawala barani Afrika kutovichukulia vyama vya upinzani kama maadui wa serikali badala yake vionekane kama moja ya nguzo muhimu katika kutimiza utawala wa sheria.

Aidha, Rais Kikwete amewataka wabunge wa vyama tawala pamoja na viongozi wengine, kuvikosoa vyama vyao pale vinapokwenda mrama badala ya kuwa waoga na kuunga mkono mambo yote.

Rais Kikwete ambaye ni maarufu Tanzania kwa jina la JK ameyasema hayo alipokuwa katika mkutano wa masuala ya uongozi barani Afrika wa mwaka 2017 (African Leadership Forum 2017) ambao umefanyikia nchini Afrika Kusini.

Viongozi wengine waliohudhuria mkutano huo ni pamoja na Rais mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa, Rais mstsaafu wa Nigeria, Olusegun Obasanjo, Rais mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki na Rais mstaafu wa Malawi, Bakili Muluzi.

No comments:

Post a Comment