KIMENUKA… RAY C AMUWAKIA NANDY

MWANAMUZIKI Rehema Chalamila ‘Ray C’ amesema hatasita kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wanamuziki wanaoimba nyimbo zake bila makubaliano

Nyota huyo ambaye kwa sasa yupo nje ya nchi ameimbia Mwananchi kuwa hawezi kuvumilia vitendo hivyo kwasababu vinalenga kumuharibia biashara yake ya muziki ambayo ndio maisha yake.

Amesema, “Muziki ni biashara huwezi ukalipwa pesa nyingi halafu ukapanda jukwaani ukaimba nyimbo za msanii mwingine bila makubaliano. Huu ni ufinyu wa ubunifu,”

Kauli hiyo ya Ray C imekuja siku moja baada ya kuandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kuwa hakufurahishwa na kitendo cha Nandy kuimba wimbo wake bila ridhaa yake.

No comments:

Post a Comment