Lowassa: Siwezi kuzuia mafuriko kwa mikono

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema kuwazuia wananchi kwenda nyumbani kwake kumshawishi agombee urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu ni sawa na kuzuia mafuriko kwa mkono.
Lowassa alitoa kauli hiyo nyumbani kwake mjini Dodoma jana wakati alipotembelewa na kundi jipya kutoka Mbarali mkoani Mbeya waliokwenda kumshawishi atangaze nia kugombea urais.
Lowassa ametoa kauli hiyo siku moja baada ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye kusema kuwa kwa kuandaa makundi ya kumshawishi, mbunge huyo wa Monduli anajua adhabu yake na anaweza kupoteza sifa za kuwa mgombea urais kupitia CCM.

No comments:

Post a Comment