HABARI KAMILI YA WATU 9 WALIOTEKETEA KWA MOTO BUGURUNI

WATU tisa wa familia moja wamekufa kwenye ajali ya moto ulioteketeza nyumba yao jijini Dar es Salaam, huku baba wa familia akinusurika kwa kuwa alikuwa amekwenda msikitini kuswali.

Nyumba hiyo iliyoteketea iko Mtaa wa Gulam katika eneo la Buguruni Malapa na baba wa familia hiyo, Masoud Matal hali yake ni mbaya. Marehemu hao walizikwa jana katika makaburi ya Kisutu.

Wakizungumza na mwandishi, majirani walisema marehemu hao walikutwa wamekumbatiana baada ya kupiga kelele kwa muda mrefu wakiomba msaada bila mafanikio kutokana na waokoaji kushindwa kupenya nyumba hiyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Lucas Mkondya, alithibitisha watoto watano na watu wazima wanne wamekufa katika kadhia hiyo. Kamanda huyo amesema kwamba chanzo cha moto ni hitilafu ya umeme, lakini alisema uchunguzi unaendelea kufahamu sababu ya moto huo.

Mashuhuda wazungumza

No comments:

Post a Comment