ADHABU SABA KWA MAWAZIRI 5 WALIOKAIDI AGIZO LA MAADILI


Pamoja na mawaziri wa tano wa Rais John Magufuli kuwasilisha fomu za tamko la rasilimali na madeni na kiapo cha uadilifu kukwepa kihunzi cha kutumbuliwa majipu na bosi wao, vigogo hao wanabanwa na adhabu saba kwa kuvunja Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma namba 13 ya mwaka 1995, ikiwamo kushushwa cheo au kusimamishwa kazi.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliwaambia wanahabari jijini hapa jana kuwa viongozi wa umma wanaoshindwa kuwasilisha fomu hizo ndani ya siku 30 zinazotakiwa kisheria, hutakiwa kutoa maelezo na iwapo hayataridhisha mamlaka husika huchukua hatua za kinidhamu.

No comments:

Post a Comment