Magufuli aagiza operesheni funga kazi

Wakati wimbi la timua timua ya watendaji wazembe na waliotumia madaraka yao vibaya likiendelea, serikali ya Rais John Magufuli pia imewageukia ombaomba wa maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam, ambapo imeagiza ifanyike operesheni kabambe ya kuwaondoa.

Operesheni hiyo inatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa na serikali imeagiza zoezi la kuwaondoa liwe limekamilika hadi kufikia Machi 10.

Ombaomba hao watasombwa hadi kwenye kambi ya JKT Ruvu, Pwani ambako watahifadhiwa kwa muda kabla ya maofisa wa Ustawi wa Jamii wa mikoa wanakotoka kuwachukua kwa mabasi ya kukodi.

Mmoja wa wafanyakazi wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, ambaye hakutaka jina lake litajwe, aliliambia gazeti hili kuwa hivi sasa vikao vya kufanikisha mkakati huo vinaendelea katika Ofisi ya Waziri Mkuu.

No comments:

Post a Comment