POLISI WAZIMA VURUGU ZA WAMACHINGA MKOANI MBEYA

 Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, limelazimika kutumia mabomu ya machozi kuzuia hali ya taharuki iliyokuwa imezuka katika maeneo ya Mwanjelwa, Kabwe hadi Soweto, jijini Mbeya, kufuatia vurugu zilizoambatana na uchomaji matairi zilizokuwa zikifanywa na wafanyibiashara ndogondogo, maarufu kama wamachinga.
 Chanzo cha sakata zima, kilikuwa zoezi lililoendeshwa na Halmashauri ya Jiji la Mbeya, la kuvunja vibanda vya wamachinga katika maeneo hayo, zoezi ambalo lilifanywa usiku wa kuamkia leo hii Februari 27.
Chanzo kimoja cha habari kimemueleza mwandishi wa mtandao huu kuwa, zoezi hilo lilifanywa ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa Jiji la Mbeya, kuweka mazingira yake katika hali ya usafi, huku ikidaiwa kuwa, wafanyibiashara hao, walishaelezwa mara kadhaa kuondoka katika maeneo hayo, lakini wakakaidi agizo la Jiji.

No comments:

Post a Comment