Taarifa ya Serikali Kuhusu Ugonjwa wa Kipindupindu

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO

TAMKO KUHUSU MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI LILILOTOLEWA NA MHE. DKT. HAMISI A. KIGWANGWALLA (MB); NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO, TAREHE 29 FEBRUARI 2016


Ndugu Waandishi wa Habari,

Taarifa hii ni mwendelezo wa utaratibu ambao Wizara yangu imejiwekea kila wiki wa kutoa taarifa kwa umma kuhusu hali ya kipindupindu nchini pamoja na kueleza juhudi mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa ili kukabiliana na hali hii. Hadi kufikia tarehe 28 Februari 2016,jumla ya wagonjwa 16,825 wametolewa taarifa, na kati ya hao watu 258 wamepoteza maisha.

Takwimu za wiki iliyopita zinaonyesha kuwa kuanzia tarehe 22 hadi 28 Februari 2016, idadi yawagonjwa wapya walioripotiwa ni 473, na kati yao watu 9 walipoteza maisha yao. Takwimu hizi za idadi ya wagonjwa katika wiki hii, zinaonyesha kuwa idadi ya wagonjwa imepungua japo kwa kiasi kidogo sana (5%) ukilinganisha na wiki iliyopita ambapo wagonjwa 499 waliripotiwa. Katika wiki iliyoishia tarehe 21 Februari, Mkoa wa Iringa ndio uliokuwa ukiongoza kwa kuwa na wagonjwa wengi zaidi. Kwa wiki hii idadi ya wagonjwa kwa mkoa huo imepungua kwa kiasi kikubwa sana japo idadi ya wagonjwa nchini kwa ujumla imeendelea kubakia kuwa juu.

No comments:

Post a Comment