DUDU JINGINE BANDARI YA DAR

Ticts ni kampuni ya kimataifa ya huduma za makontena inayosimamia na kuhifadhi makontena katika bandari ya Dar es Salaam.Pia ni mwanachama wa kampuni ya kimataifa ya CK Hutchison Holdings inayofanya kazi katika bandari 52 kwenye nchi 26 duniani. 

Baada ya kuibuka sakata la mita za kupimia mafuta na ukwepaji wa kodi kwa makontena bandarini, Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) imebainisha kashfa nyingine kwenye kitengo cha mizigo kinachoendeshwa na Kampuni ya Kimataifa ya Huduma za Makontena (Ticts).
Ripoti hiyo iliyotolewa mapema wiki hii imebaini Ticts imevunja taratibu za mkataba na hivyo kusababisha kuikosesha mapato Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA).
CAG Mussa Juma Assad ameonyesha katika ripoti ya ukaguzi wa mashirika ya umma kuwa Ticts ilianza kuvunja makubaliano ya mkataba na TPA baada ya kubadilisha umiliki wa asilimia 51 wa hisa za Ictis zilizoko kampuni ya Ticts kwenda Hutchison International Port Limited (HPH).

No comments:

Post a Comment