SUKARI: MTIHANI WA KWANZA SERIKALI YA MAGUFULI KUFELI

By Malisa GJ,
Takribali Miezi miwili iliyopita Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.John Pombe Magufuli alipiga marufuku uingizwaji wa sukari nchini kwa madai ya kusaidia kulinda viwanda vya ndani vinavyozalisha biidhaa hiyo nchini. Rais Magufuli alitoa agizo hilo wakati akizungumza na wafanyabiashara ambapo alitaka agizo hilo lianze kutekelezwa mara moja.

Baada ya utekelezaji wa agizo hilo kuanza kumejitokeza mfumuko mkubwa wa bei katika bidhaa ya sukari ambayo imepanda kutoka Shilingi 1,800/= kwa kilo moja hadi shilingi 2500/- huku baadhi ya maeneo ikifika shilingi 2800/-. Ongezeko hili ni wastani wa asilimia 39% hadi 55% kwa kilo moja ya sukari. Yani mfumuko wa bei ya sukari umefikia asilimia 55% ndani ya kipindi kisichiozidi miezi miwili. Hii ni ishara mbaya sana kiuchumui (Indicator for galloping inflation).

Kwanini Rais alizuia sukari kutoka nje?
Rais Magufuli alipiga marufuku uingizwaji wa sukari ya nje ili kuilinda viwanda vya ndani. Kiuchumi bidhaa kutoka nje inaweza kuathiri viwanda vya ndani (infant industries) vinavyozalisha bidhaa kama hiyo, hasa ikiwa bidhaa hizo za nje zitauzwa kwa bei ndogo kuliko zinazozalishwa nchini. Hii inaitwa Protectionism theory.!

No comments:

Post a Comment