Manara Atangaza Kumposa Wema Sepetu


Haji Manara (Kushoto), Wema Sepetu (Kulia).
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Haji Sunday Manara amelipa mtihani mwingine Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kuahidi kufanya maamuzi makubwa endapo ratiba ya ligi kuu haitabadilishwa hadi mwisho wa msimu.
Maamuzi ambayo Haji ametangaza kuyafanya ni kumposa mrembo wa Tanzania (Miss Tanzania) mwaka 2006 Wema Sepetu na kumuoa endapo atakubali, lakini kama hatakubali, Haji ameahidi kutembea akiwa amevaa nguo ya ndani pekee (Boxer) kutoka nyumbani kwake hadi katika ofisi za TFF zilizoko Ilala Dar es Salaam.
“Nimalizie Kwa kuwapa mtihani mwingine TFF na bodi ya Ligi, iwapo Kama ratiba yao ya Ligi kuu na Kombe la shirikisho haitabadilishwa kuanzia sasa hadi mwisho wa msimu, ntamposa mlimbwende Wema Sepetu, na akikubali ntamuoa, akikataa ntatembea na boxer toka Nyumbani kwangu hadi TFF” Amesema Manara

No comments:

Post a Comment