MWANAMKE WA KITANZANIA AUWAWA KINYAMA UINGEREZA

MTANZANIA Leyla Mtumwa (36) mkazi wa Arusha aliyekuwa akiishi Uingereza anadaiwa kuuawa kwa kuchomwa visu sehemu mbalimbali za mwili wake na mwanaume mwenye umri wa miaka 38 (jina halijatajwa) ambaye pia ni Mtanzania anayesemekana kuwa ni mpenzi wake waliokuwa wakiishi naye pamoja.

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea usiku wa kamkia jana Machi 30, 2018, katika nyumba wanayoishi Watanzania hao iliyopo eneo la Haringey, Kirkstall Avenue, N17 jijini London, baada ya kuzuka ugomvi baina yao ikiwa ni muda mfupi baada Leyla kurejea nyumbani akitokea disco la usiku alikokuwa amekwenda na marafiki zake.

Vyanzo mbalimbali vinaeleza kuwa, alirudi kutoka disco akiwa na rafiki yake wamelewa na kuingia ndani, ambapo alimkuta mpenzi wake ambaye alianza kufoka na kutukana jambo lililoibua mzozo mkali baina yao.

No comments:

Post a Comment