Rais Kenyatta apingwa Israel

Jerusalem, Israel. Chama cha ukombozi wa Palestina (PLO) kimepinga ziara ya Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya katika Jerusalem ya mashariki na sehemu ya makazi ya Israel katika ukingo wa magharibi wa Mto Jordan.

Kamati ya utendaji ya PLO imesema makubaliano ya kimataifa yanataja ardhi ya Palestina iliyotawaliwa na Israel mwaka 1967 ni ardhi ya nchi ya Palestina na siyo vinginevyo.

Rais Kenyatta yuko katika ziara ya kiserikali nchini Israel. Hii ni ziara yake ya kwanza kwa Rais Kenyatta kufanyika nchini hapa wakati mataifa hayo yakiwa katika mkakati wa kuimairisha uhusiano wa kibiashara.

No comments:

Post a Comment